KM ahimiza maendeleo ya haraka Kenya kwenye mazungumzo ya upatanishi
Msemaji wa Katibu Mkuu, Michele Montas amearifu kwenye mkutano wa hadhara ya kwamba Katibu Mkuu Ban Ki-moon ametoa risala yenye kuhimiza yale makundi yanayohusika na Mazungumzo ya Taifa na Upatanishi Kenya, kufanya kila wawezalo, na kuchukua hatua za haraka, kuhakikisha watafikia suluhu ya kuridhisha juu ya mfarakano uliolivaa taifa lao.