Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Khofu ya kurejea makwao inawasumbua Wakenya waliokimbilia Uganda

Khofu ya kurejea makwao inawasumbua Wakenya waliokimbilia Uganda

UNHCR imeripoti kwamba asilimia kubwa ya raia 12,000 wa Kenya waliovuka mpaka na kwenda Uganda kupata hifadhi, baada ya machafuko kuzuka nchini kufuatia uchaguzi wa Disemba 27 mwaka jana, kuwa wanakhofu kurejea makwao kwa hivi sasa, licha ya kuwa ripoti za jamii ya kimataifa zilithibitisha hali ya usalama, kwa ujumla, nchini imeanza kutengenea.