Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Raia wa Chad waliokimbilia Cameroon wahamishwa tena kwenye kambi mpya

Raia wa Chad waliokimbilia Cameroon wahamishwa tena kwenye kambi mpya

Shirika la Umoja wa Mataifa juu ya huduma za Wahamiaji (UNHCR) limeripoti wahamiaji 5,500 waliokimbia mapigano mwanzo wa mwezi kutoka mji wa N’Djamena, Chad na ambao walikuwa wakiishi kwenye makazi ya muda kaskazini-mashariki ya Cameroon, hivi sasa wamepelekwa uhamishoni kwenye kambi mpya ziliopo kijiji cha Maltam, kitendo ambacho kinatazamiwa kurahisisha ugawaji wa misaada ya kihali kwa umma husika kutoka mashirika ya kimataifa.Kadhalika uhamisho huu utayawezesha mashirika yanayohusika na misaaada ya kiutu kuwapatia wahamiaji hawo hifadhi kinga. Jumla ya wahamiaji 30,000 wa Chad hivi sasa wanaishi kwenye maskani ya muda katika eneo la Cameroon kaskazini.