Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

WFP imeanza kugawa chakula Bukini kwa waathiriwa wa Tufani Ivan

WFP imeanza kugawa chakula Bukini kwa waathiriwa wa Tufani Ivan

Shirika la Umoja wa Mataifa juu ya Miradi ya Chakula Duniani (WFP) limeanzisha huduma za dharura za kugawa chakula katika yale maeneo ya Bukini yaliodhirika na uharibifu wa Tufani Ivan iliopiga wiki iliopita. Makumi elfu ya watu wanategemea misaada hiyo ya kihali kutoka mashirika ya UM, hususan ule umma unaoishi kwenye mahema mjini Antananarivo, ambao nyumba zao ziliharibiwa na tufani, pamoja na wale watu wanaoishi kwenye sehemu za mwambao wa mashariki ya Bukini na kwenye kisiwa cha St. Marie, maeneo yalioumia zaidi na gharika ya Tufani Ivan.