Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

DPKO inakhofia wanajeshi wa UNAMID hawatoenezwa Darfur kwa wakati

DPKO inakhofia wanajeshi wa UNAMID hawatoenezwa Darfur kwa wakati

Jean-Marie Guehenno, Mkuu wa Idara ya UM juu ya Operesheni za Ulinzi wa Amani Duniani (DPKO), alikuwa na mashauriano maalumu na wajumbe wa Baraza la Usalama kuhusu vizingiti vilivyoibuka kwenye juhudi za kukamilisha upelekaji wa vikosi mseto vya UNAMID katika jimbo la Darfur, Sudan magharibi. Vikosi vya UNAMID vinategemea mchango wa wanajeshi wa Umoja wa Mataifa (UM) na Umoja wa Afrika (UA).