Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mashirika ya UM yaendelea kuhudumia misaada ya kiutu Kenya

Mashirika ya UM yaendelea kuhudumia misaada ya kiutu Kenya

UM na mashirika yake mbalimbali yaliopo Kenya yanashiriki kwenye huduma kadha wa kadha za kukidhi mahitaji ya umma ulioathiriwa na machafuko yaliyofumka karibuni nchini Kenya baada ya uchaguzi kumalizika. Kwa mujibu wa taarifa ya Ofisi ya UM juu ya Misaada ya Dharura (OCHA) misaada hii hugaiwa na kuenezwa kwenye maeneo muhitaji na mashirika ya UM, mathalan UNHCR, WFP na UNICEF, hususan katika lile eneo la Kaskazini la Mkoa wa Bonde la Ufa/Northern Rift Valley.

Sikiliza mahojiano kamili kwenye idhaa ya mtandao.