Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

KM atathminia shughuli za UM kwa 2008

KM atathminia shughuli za UM kwa 2008

KM Ban Ki-moon alikutana na waandishi habari mwanzo wa wiki na aliwasilisha ajenda aliyopendekeza ijumuishwe katika kazi za UM katika mwaka 2008. KM Ban alisema kwenye risala yake ya ufunguzi kwamba atatumia wadhifa wake kuhakikisha 2008 utakaobarikiwa mchango ziada kutokana na bidii ya kimataifa katika kukabiliana na masuala yanayohusu mabadiliko ya hali ya hewa duniani na pia ulinzi wa amani ya kimataifa.~~