Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mradi wa Mbola kupiga vita umasikini kwa kuwaridhisha madaraka wanakijiji

Mradi wa Mbola kupiga vita umasikini kwa kuwaridhisha madaraka wanakijiji

Mradi wa Umoja wa Mataifa wa Vijiji vya Milenia (MVP) unaotekelezwa kwenye Kijiji cha Mbola, Tanzania unajitahidi kuwasaidia wanakijiji kupatiwa madaraka na uwezo wa kujiamulia taratibu zinazofaa kuhudumiwa kupunguza umasikini na hali duni kwenye eneo lao. Huduma hizi huongozwa na wataalamu wa fani mbalimbali ambao huwasaidia wanakijiji kupata ujuzi unaowaletea natija za kiuchumi na, hatimaye, kuwavua na janga la umasikini na ufukara. Katika kipindi tumebahatika kujumuisha maoni ya mwanakijiji Christina Mabula pamoja na Anna Linje, mwanafunzi mtafiti wa Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine, kiliopo Morogoro, Tanzania ambayo yanazingatia juhudi zinazotakikana kuimarisha kipamoja maendeleo ya kijijini katika Mbola.