Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mjumbe Mpya wa UM kwa Liberia amewasili kuanza kazi

Mjumbe Mpya wa UM kwa Liberia amewasili kuanza kazi

Mjumbe Maalumu mpya wa KM kwa Liberia, Ellen Margrethe Loj wa Denmark amewasili Liberia kuanza kazi, na aemahidi kulisaidia taifa husika la Afrika Magharibi kuimarisha amani, utulivu na demokrasia katika kipindi cha mpito baada ya vita vya wenyewe kwa wenyewe vya miaka kumi kusitishwa nchini. ~~Bi Loj alisema ijapokuwa mafanikio kadha yameshuhudiwa baada ya mapigano kusita, hata hivyo badio kuna majukumu mbalimbali yanayohitajia kushughulikiwa kuupatia umma wa Liberia utulivu wanaohitajia kuendeleza maisha yao ya kawaida.