Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UNICEF kuiombea Malawi msaada wa dharura kudhibiti mafuriko

UNICEF kuiombea Malawi msaada wa dharura kudhibiti mafuriko

Shirika la UM kuhusu Mfuko wa Maendeleo kwa Watoto (UNICEF)limetangaza ombi maalumu linaloishinikiza jumuiya ya kimataifa kufadhilia mchango wa dharura wa dola milioni 2.5 kuhudumia chakula ule umma ulioathirika na mafuriko yaliosambaa Malawi. UNICEF imetahadharisha kwenye taarifa yake kwamba pindi ombi lao halitokamilishwa kwa wakati kuna hatari ya watu milioni moja kukabiliwa na njaa maututi katika Malawi.