Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Watu 500,000 waling'olewa makwao mwaka jana DRC, UM yathibitisha

Watu 500,000 waling'olewa makwao mwaka jana DRC, UM yathibitisha

Ofisi ya UM juu ya Misaada ya Dharura (OCHA) imeripoti kwamba katika miezi 12 iliopita watu nusu milioni waling’olewa makwao katika Jamhuri ya Kidemokrasiya Kongo (DRC) kwa sababu ya kuselelea kwa mapigano baina ya Jeshi la Taifa (FARDC) na makundi ya waasi na wanamgambo, hali ambayo haijawahi kushuhudiwa tangu 2003 pale vita vya wenyewe kwa wenyewe viliposhtadi kwa wingi nchini humo.