Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mjumbe Mpya wa KM katika JKK akutana na viongozi kuzungumzia amani

Mjumbe Mpya wa KM katika JKK akutana na viongozi kuzungumzia amani

Alan Doss, Mjumbe Maalumu mpya wa Katibu Mkuu katika Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo (DRC) amekutana majuzi na Raisi Joseph Kabila pamoja na maofisa wa serikali mjini Kinshasa ambapo walizingatia kipamoja masuala yanayohusu shughuli za ulinzi wa amani katika DRC.