Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UM imeanzisha operesheni za kuwasaidia waathiriwa wa mafuriko kusini ya Afrika

UM imeanzisha operesheni za kuwasaidia waathiriwa wa mafuriko kusini ya Afrika

Ofisi ya UM inayohusika na Misaada ya Dharura (OCHA) imeripoti kuongezeka kwa kiwango cha mara mbili idadi ya watu waliong’olewa makwao, kusini ya Afrika kutokana na mafuriko, katika kipindi cha wiki moja na kufikia 120,000 ziada. Hivi sasa Shirika la UM juu ya Miradi ya Chakula Duniani (WFP) linasaidia kuhudumia misaada ya chakula Msumbiji, kwa kutumia helikopta, kwa waathirwa wa mafuriko 13,000 waliopatiwa makazi ya muda kwenye kambi za wahamiaji.