Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

WaSomali 130 ziada wafariki baada ya mashua yao kupinduka Yemen

WaSomali 130 ziada wafariki baada ya mashua yao kupinduka Yemen

Shirika la UM Linalohudumia Wahamiaji (UNHCR) limeripoti watu 130 ziada kutoka Usomali, wingi wao wakikimbia vurugu na fujo nchini mwao, walifariki mwisho wa wiki pale mashua yao ilipopinduka karibu na mwambao wa Yemen. Wahamiaji hawa walipigwa visu na magongo na kudhalilishwa na wale wafanyabiashara ya magendo ya kuvusha watu. Wingi ya wahamiaji walizama kwa sababu ya hali mbaya ya hewa iliosababisha mawimbi makali kupindua mashua yao.