Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Taadhima ya Geneva inawakumbuka watumishi wa UM waliouawa Algiers

Taadhima ya Geneva inawakumbuka watumishi wa UM waliouawa Algiers

KM Ban Ki-moon, akijumuika na watumishi wa UM Geneva walifungua taadhima ya kuwaheshimu na kuwakumbuka wafanyakazi wenziwao 17 waliouawa na bomu la kujitolea mhanga Algeria mwezi uliopita, kwa kusimama kimya kwa dakika moja. Baada ya hapo KM alifunua rasmi ile bendera iliohifadhiwa ndani ya kioo kilichozungukwa na ubao wa matangazo, bendera ambayo ndio iliokuwa ikipeperuka kwenye ofisi za UM Algiers, na ilioraruliwa na kuchanwa na bomu la magaidi. KM alikabidhiwa bendera hiyo alipozuru ofisi za UM Algiers, siku chache baada ya tukio la magaidi kujiri.