Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Hapa na pale

Hapa na pale

Katika tafrija ya kutathminia Mafanikio ya Mfuko wa Maendeleo ya MDGs mjini NY, Naibu KM Asha-Rose Migiro alisema kwenye risala yake kwamba Malengo ya Maendeleo ya Milenia (MDGs) yametubarikia “ramani ya aina pekee” kutumiwa kujenga ulimwengu bora na alitahadharisha, vile vile, kutopwelewa katika kuzitekeleza, kwa wakati, zile ahadi za kupunguza hali duni, njaa, maradhi na kutojua kusoma na kuandika katika nchi masikini kabla ya 2015.