Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UNICEF kuchanja watoto na wanawake 100,000 Somalia dhidi ya maradhi

UNICEF kuchanja watoto na wanawake 100,000 Somalia dhidi ya maradhi

Shirika la UM juu ya Mfuko wa Maendeleo kwa Watoto (UNICEF) limeanzisha huduma ya kuchanja watoto wachanga 47,000 walio chini ya umri wa miaka mitano pamoja na wanawake 56,000 wanaoishi kwenye kambi za wahajiri wa ndani ya nchi ziliopo kwenye eneo la Mogadishu-Afgooye, katika Usomali. Huduma hii itasaidia kuupatia umma husika tiba ya kingamaradhi dhidi ya magonjwa yanayosababishwa na ukosefu wa mastakimu ya kawaida.