Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mapigano Chad yakwamisha misaada ya kiutu kupelekewa umma muhitaji

Mapigano Chad yakwamisha misaada ya kiutu kupelekewa umma muhitaji

Ofisi ya UM inayohusika na Misaada ya Dharura (OCHA) imeripoti kuingiwa na wasiwasi mkuu kuhusu usalama wa wahamiaji wa Sudan 230,000 pamoja na wahajiri wa ndani ya nchi 180,000 nchini Chad kwa sababu ya kuselelea hali ya mapigano katika eneo la Chad mashariki. Vurugu hili, ilisema ripoti ya OCHA, linakwamisha huduma za dharura za kupeleka misaada ya kiutu inayohitajika kunusuru kihali umma huo.