Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Naibu KM apongeza utaratibu mpya wa kuimarisha amani Burundi

Naibu KM apongeza utaratibu mpya wa kuimarisha amani Burundi

Naibu KM Asha-Rose Migiro majuzi alishiriki kwenye mjadala wa Kamisheni ya UM juu ya Ujenzi wa Amani uliofanyika Makao Makuu ya UM ambapo kulizingatiwa mfumo mpya wa kurudisha utulivu na amani Burundi. Katika risala yake mkutanoni Naibu KM aliipongeza Burundi kwa kujishurutisha kutekeleza mpango wa amani nchini baada ya mapigano ya zaidi miaka kumi kusitishwa.