Skip to main content

"Jamii ya kimataifa yawajibika kuisaidia Afrika kutatua matatizo ya mipaka" - Ban Ki-moon

"Jamii ya kimataifa yawajibika kuisaidia Afrika kutatua matatizo ya mipaka" - Ban Ki-moon

Katika risala aliyotuma kwenye Warsha wa Umoja wa Afrika Kuzingatia Suluhu ya Mizozo ya Mipaka, uliofanyika Disemba mosi nchini Djibouti, KM Ban Ki-moon alitoa mwito maalumu wenye kuihimiza jumuiya ya kimataifa kupania kuzisaidia nchi za Afrika kusuluhisha matatizo ya mipaka kwa taratibu za kuridhisha na kudumisha mistari halali ya mipaka yao na, hatimaye, kujiepusha na hatari ya kutumia masuala hayo siku za usoni kama kisingizio cha kufufua tena mapigano na vurugu kwenye maeneo yao.