Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mjumbe Maalumu wa UM ameahidi kuongeza kasi kuwasilisha amani Darfur

Mjumbe Maalumu wa UM ameahidi kuongeza kasi kuwasilisha amani Darfur

Mjumbe Maalumu wa KM kwa Darfur, Jan Eliasson aliwaambia waandishi habari mjini Khartoum, Sudan kwamba Umoja wa Mataifa na Umoja wa Afrika watajitahidi sana, katika wiki chache zijazo, kuongeza kasi ya mashauriano yatakayosaidia kuharakisha mazungumzo ya kurudisha utulivu na amani kati ya Serikali ya Sudan na makundi kadhaa ya waasi kutoka jimbo la magharibi ya nchi la Darfur.