Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

KM ahimiza mataifa yakubaliane na ajenda ya Bali

KM ahimiza mataifa yakubaliane na ajenda ya Bali

Kwenye Mkutano Mkuu wa UM juu ya Udhibiti wa Mabadiliko ya Hali ya Hewa duniani, unaofanyika Bali, Indonesia KM Ban Ki-moon alitahdaharisha wajumbe wa kimataifa kwamba suala la athari zinazoletwa na mabadiliko ya hewa ni "tatizo linalotatanisha sana maadili halisi ya vizazi vya leo" na kwamba tusahau "macho yote ya ulimwengu yanasubiri kuona hatua gani za kuridhisha zitachukuliwa na jamii yetu kulisuluhisha tatizo hili kuu la karne ya sasa."