Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Baraza Kuu laahidi kujenga ulimwengu salama kwa watoto

Baraza Kuu laahidi kujenga ulimwengu salama kwa watoto

Baraza Kuu la UM Alkhamisi limepitisha kwa sauti, na kauli moja, azimio la msingi ambalo Mataifa Wanachama yameahidi kukamilisha malengo ya kuendeleza maisha bora kwa watoto, hasa katika kuwapatia afya na elimu yenye natija kimaisha, na kuwapatia hifadhi inayofaa dhidi ya unyanyasaji, mateso na utumiaji nguvu, na pia kuwahakikishia udhibiti bora na tiba kinga dhidi ya UKIMWI/VVU.