21 Disemba 2007
Ahmedou Oul-Abdallah, aliye Mjumbe Maalumu wa KM kwa Usomali aliwaambia wawakilishi wa katika Baraza la Usalama wiki hii, kwenye mkutano wa hadhara, ya kwamba wakati umeshawadia kwa wao kuandaa ramani hakika ya kidiplomasiya, ili kuisaidia Usomali kurudisha tena hali ya utulivu na amani nchini.