Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UNHCR yahimiza mapigano yakomeshwe Kivu Kaskazini kunusuru raia

UNHCR yahimiza mapigano yakomeshwe Kivu Kaskazini kunusuru raia

Antonio Gutteres, Kamishna Mkuu wa Shirika la UM juu ya Huduma za Wahamiaji (UNHCR) ambaye alizuru Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo (JKK)hivi karibuni, ametoa mwito wenye kuyanasihi makundi yote yalioshiriki kwenye uhasama na mapigano katika jimbo la Kivu Kaskazini, kusitisha mapigano haraka iwezekanavyo, hali ambayo ikikamilishwa itayawezesha mashirika ya kimataifa yanayofadhilia misaada ya kiutu kupata fursa ya kuhudumia kihali umma muhitaji ulionaswa kwenye mazingira ya mapigano.