Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Asilimia kubwa ya watoto walionyakuliwa Chad wanaishi na wazee

Asilimia kubwa ya watoto walionyakuliwa Chad wanaishi na wazee

Mashirika ya UM, ikijumuisha lile shirika linalohusika na mfuko wa maendeleo ya watoto, UNICEF na lile linalosimamia huduma za wahamiaji, UNHCR yakichanganyika na Kamati ya Kimataifa ya Msalaba Mwekundu, ICRC yameripoti kwa kauli moja ya kuwa wale watoto 103 waliotuhumiwa kuibiwa hivi karibuni nchini Chad, kwa madai walikuwa ni watoto mayatima wanaohitaji familia za kuwatizama kihali na mali imebainika kihakika, baada ya uchunguzi kufanyika na wahudumia misaada ya kiutu kwamba kati ya idadi hiyo watoto 91 walikuwa na wazee wao halali na sio mayatima abadan. Watoto 12 waliosailia sasa hivi wanaendelea kufanyiwa uchunguzi ziada kutafutiwa wazee wao na kuthibitisha kama ni mayatima au la.