Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Baraza la Usalama laongeza muda wa UNMIS kuimarisha amani Sudan

Baraza la Usalama laongeza muda wa UNMIS kuimarisha amani Sudan

Baraza la Usalama limepitisha azimio la kuongeza kwa miezi sita zaidi operesheni za kulinda amani za UNMIS. Shirika la UNMIS ni taasisi ya UM inayosimamia kusitishwa mapigano ya miaka 21 kati ya Sudan kusini na kaskazini.