Vikosi vya UNAMID vyaanzisha operesheni mpya Darfur
Vikosi vya mseto vya UM/UA kulinda amani katika Darfur, yaani vikosi vya UNAMID vilianzisha rasmi operesheni zake katika jimbo hilo la Sudan Magharibi mnamo mwisho wa Oktoba. Operesheni hizo zinaambatana na ufunguzi wa Makao Makuu ya UNAMID kwenye mji wa El Fashir.