IFAD kusaidia wanavijiji masikini Lesotho
Shirika la UM juu ya Mfuko wa Kimataifa kwa Maendeleo ya Kilimo (IFAD) limeanzisha mradi mpya wa dola milioni 8.7 kusaidia wanavijiji masikini 37,000 katika Lesotho. Mradi huu utawafadhilia wanavijiji husika mchango wa fedha za kuekeza kilimo chenye natija kiuchumi na kijamii kwenye maeneo yao.