Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Makamanda waasi katika Ituri, DRC wahamishwa Kinshasa na UM

Makamanda waasi katika Ituri, DRC wahamishwa Kinshasa na UM

Shirika la Ulinzi wa Amani la UM katika JKK (MONUC) limeripoti kufanikiwa kuwahamishia kwenye mji wa Kinshasa wale makamanda 16 waliokuwa wakiongoza makundi ya waasi katika eneo la Ituri. Kitendo hiki, ilisema MONUC, ni hatua kubwa katika kurudisha utulivu wa kijamii na kuimarisha amani kwenye jimbo la uhasama la kaskazini-mashariki ya nchi.