Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Afisa wa UM anasema waasi wa Darfur hawakunyimwa fursa ya kushiriki kwenye mpango wa amani

Afisa wa UM anasema waasi wa Darfur hawakunyimwa fursa ya kushiriki kwenye mpango wa amani

Ofisa Mkuu wa Habari katika UM, Ahmad Fawzi ambaye alihudhuria mazungumzo ya amani kwa Darfur yaliofanyika Sirte, Libya alipokutana na waandishi habari mjini New York wiki hii, baada ya kurejea mkutanoni, alisisitiza ya kwamba “fursa ya kushiriki kwenye mpango wa kurudisha amani Darfur bado ipo kwa yale makundi ya waasi wasiohudhuria kikao cha Sirte, pindi makundihayo yatakuwa tayari kujiunga kidhati na utaratibu huo.”