Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Burundi yapongezwa na UM kwa kuunda serikali mpya

Burundi yapongezwa na UM kwa kuunda serikali mpya

Ofisi ya UM Inayosimamia Huduma za Amani Burundi (BINUB) pamoja na wawakilishi wa jumuiya ya kimataifa waliopo nchini humo wamepongeza maafikiano ya karibuni ya wanasiasa kwa mchango wao uliowezesha serekali mpya kuundwa, pamoja na kiongozi wa nchi kuteuliwa. Viongozi wote wa Burundi wamenasihiwa na UM kuchukua hatua zote muhimu ili kuhakikisha demokrasia inaimarishwa na kudumishwa kwenye taifa lao.