Demokrasia inaanza kushika mizizi DRC, asema KM Ban
Katika ripoti ya UM iliowasilishwa karibuni kusailia hali katika JKK (DRC) KM Ban Ki-moon alithibitisha kwamba usalama wa taifa uliathiriwa nchini na haki za binadamu ziliharamishwa kwa sababu ya kuzuka migogoro miwili; kwanza, uhasama uliochipuka, baada ya kufanyika uchaguzi, baina ya serikali na wafuasi wa Makamu Raisi wa zamani, Jean-Pierre Bemba na, pili, mikwaruzuano ilioselelea kieneo kati ya Jeshi la Taifa na wanajeshi waasi, ambao huongozwa na Jenerali aliyetoroka jeshi Laurent Nkunda.