Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Raia wa Afrika Kusini kuongoza operesheni mseto za polisi Darfur

Raia wa Afrika Kusini kuongoza operesheni mseto za polisi Darfur

Michael J. Fryer wa Afrika Kusini ameteuliwa rasmi na Mwenyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika (AU), baada ya kushauriana na KM wa UM Ban Ki-moon, kuwa Kamishna wa Polisi wa operesheni mseto za ulinzi wa amani katika Darfur. Operesheni hizi zitaendelezwa shirika kati ya Umoja wa Mataifa na Umoja wa Afrika (UM/UA), na kuongozwa na Shirika la UNAMID.