Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Siku ya Kuimarisha Haki kwa Watoto Duniani.

Siku ya Kuimarisha Haki kwa Watoto Duniani.

Tarehe 20 Novemba kila mwaka huadhimishwa na Mataifa Wanachama kuwa ni siku ya kukumbushana jukumu adhimu lilioikabili jumuiya ya kimataifa la kuwatekelezea watoto haki zao halali. Tangu mwaka 1989, pale Baraza Kuu la UM lilipoidhinisha Mkataba juu ya haki za Mtoto, umma wa kimataifa ulijitahidi sana kuwatekelezea watoto haki zao za kimsingi. Lakini maendeleo yaliopatikana yalikuwa haba sana na hayakuridhisha kikamilifu, hususan katika utekelezaji wa haki hizo kwa wale watoto wanaojikuta wamenaswa kwenye mazingira ya uhasama na mapigano.~~ Sikiliza ripoti kamili juu ya suala hili, kwenye idhaa ya mtandao, kutoka A. Aboud wa Redio ya UM.