Mtaalamu wa haki za binadamu anakhofia upungufu wa uhuru wa dini Angola
Asma Jahangir, Mkariri Maalumu anayehusika na masuala ya uhuru wa dini na itikadi alizuru Angola karibuni kwa wiki moja. Baada ya kumaliza ziara yake Jahngir aliripoti kwamba licha ya kuwa katiba ya taifa inaruhusu uhuru wa kuabudu na kufuata itikadi za dini mbalimbali kwa raia, aligundua kwamba baadhi ya vikundi vya Kikristo pamoja na jamii ya Kiislamu katika Angola bado wanaendelea kubaguliwa kisheria.