Mkuu wa UNDOC ahimiza hatua za haraka kupambana na wizi wa watoto Afrika
Antonio Maria Costa, Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya UM juu ya Udhibiti wa Uhalifu na Madawa ya Kulevya (UNDOC) amezihimiza serekali za Afrika ya Magharibi na Kati kuongeza huduma za usalama zinazohitajika kuwakinga watoto dhidi ya hatari ya kutekwa nyara na baadaye kuuzwa kwenye soko la kimataifa kuhudumia utumwa mamboleo.