Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

John Holmes, Mkuu wa OCHA ameanza ziara ya siku tisa Afrika

John Holmes, Mkuu wa OCHA ameanza ziara ya siku tisa Afrika

Naibu KM juu ya Misaada ya Dharura, John Holmes ameanza ziara ya siku tisa Afrika na alitazamiwa kuzuru Ethiopia, Sudan na Kenya. Holmes atakutana kwa mashauriano na wawakilishi wa mashirika ya kimataifa yanayohudumia misaada ya kiutu pamoja na maofisa wa UM, na pia wanadiplomasiya waliopo kwenye nchi anazozuru kushauriana juu ya hatua zinazofaa kuchukuliwa shirika, ili kuwanusuru kimaisha mamilioni ya watu walioathirika kihali kutokana na mifumko ya vurugu liliotanda kwenye maeneo yao katika siku za karibuni.