Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Liberia inastahili msaada wa Mfuko wa Ujenzi wa Amani: asema KM

Liberia inastahili msaada wa Mfuko wa Ujenzi wa Amani: asema KM

KM Ban Ki-moon amepitisha mwito unaothibitisha kwamba Liberia inastahili kupokea msaada wa fedha za maendeleo kutoka Mfuko wa UM juu ya Ujenzi wa Amani. Kadhalika KM ameliamrisha Shirika la Ulinzi wa Amani la UM katika Liberia (UNMIL) lianze kushauriana na wenye madaraka Liberia pamoja na mashirika ya kiraia na kuandaa ni miradi gani itafaa kupewa umbele katika kupokea misaada hiyo ya UM.