Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UM unaomba msaada wa kuhudumia kihali waathiriwa 75,000 wa mafuriko Ghana

UM unaomba msaada wa kuhudumia kihali waathiriwa 75,000 wa mafuriko Ghana

UM na washirika wake kadha wametoa mwito maalumu kwa jamii ya kimataifa unaopendekeza wafadhiliwe haraka dola milioni 10 ili kuhudumia afya, makazi na vifaa vya nyumba kwa watu 75,000 walioathirika na mafuriko Ghana kaskazini. Mafuriko haya yalioselelea tangu Agosti yalisababishwa na maji kujaa kwenye Mito ya Volta Nyeupe na Nyeusi.