Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Ghana kuongoza Baraza la Usalama kwa mwezi Oktoba

Ghana kuongoza Baraza la Usalama kwa mwezi Oktoba

Ghana imekabidhiwa uraisi wa Baraza la Usalama kwa mwezi Oktoba. Mwakilishi wa Kudumu wa Ghana katika UM, Balozi Leslie Kojo Christian aliitisha mkutano wa waandishi habari wa kimataifa katika Makao Makuu ambapo aliwaarifu kuhusu ajenda ya vikao vijavyo kwa mwezi Oktoba. Balozi Christian alidhihirisha ya kuwa ajenda ya mijadala italenga zaidi yale matatizo yanayohusu hali katika Usomali na Cote d’Ivoire, na pia alitarajia kusailiwa masuala juu ya haki za wanawake, pamoja na mada zinazoambatana na juhudi za kimataifa za kuimarisha usalama na amani duniani.