Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mahkama Maalumu Sierra Leone yatoa hukumu kwa Wanamgambo

Mahkama Maalumu Sierra Leone yatoa hukumu kwa Wanamgambo

Mahakama Maalumu kwa Sierra Leone, inayoungwa mkono kikazina UM, imepitisha hukumu ya kifungo cha miaka sita kwa Moinina Fofana, na pia kutoa adhabu ya kifungo cha miaka minane kwa Allieu Kondewa, viongozi wawili wa kundi la wanamgambo wa CDF, waliotuhumiwa kushiriki kwenye jinai ya vita pale Sierra Leone ilipokuwa imezama kwenye mapigano ya wenyewe kwa wenyewe yalioshtadi kwa muda wa miaka kumi nchini.