11 Oktoba 2007
Wiki hii Mjumbe Maalumu wa KM kwa Darfur, Jan Eliasson alikuwa na mazungumzo na viongozi mbalimbali wa hadhi ya juu wa Serekali ya Sudan, pamoja na viongozi wa mataifa jirani ikiwa katika juhudi za kimataifa za kukamilisha matayarisho ya mkutano mkuu ujao wa kurudisha amani katika Darfur, kikao ambacho kinatarajiwa kufanyika Libya tarehe 27 Oktoba (2007).