Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Silaha zinaendelea kumiminikia Darfur na kukiuka vikwazo vya UM

Silaha zinaendelea kumiminikia Darfur na kukiuka vikwazo vya UM

Tume ya wataalamu waliodhaminiwa na UM madaraka ya kusimamia utekelezaji wa vikwazo vya silaha dhidi ya Sudan imeripoti kugundua kwamba silaha nzito, silaha ndogo ndogo na vifaa vyengine vya kivita bado vinaendelea kupelekwa jimbo la Darfur. Vitendo hivi vinaendelezwa na Serekali ya Sudan pamoja na makundi ya waasi, hali ambayo inaharamisha vikwazo vya Baraza la Usalama dhidi ya silaha kupelekwa kwenye eneo hili la Sudan magharibi.