Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mandalizi ya UNAMID Darfur yanatathminiwa na KM

Mandalizi ya UNAMID Darfur yanatathminiwa na KM

Ripoti ya KM kuhusu maendeleo katika juhudi za kuandaa vikosi vya mseto vya UM na Umoja wa Afrika (AU) vitakavyopelekwa Darfur, yaani Vikosi vya UNAMID, imebainisha kupwelewa kwa sasa kwa sababu ya kuzuka vizingiti katika kupata eneo la ardhi katika Darfur linalohitajika kujenga ofisi na makazi. Kadhalika ripoti ilisema Serekali ya Sudan bado inavuta wakati kuidhinisha ile orodha waliopelekwa ya wanajeshi wa mataifa yaliojitolea kujiunga na vikosi vya ulinzi wa amani vya UM katika Darfur vya UNAMID.