Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Migiro atoa mwito wa kukithirisha uekezaji dhidi ya vifo vya uzazi

Migiro atoa mwito wa kukithirisha uekezaji dhidi ya vifo vya uzazi

Naibu KM Asha-Rose Migiro aliwaambia wajumbe waliohudhuria mkutano wa London kuhusu haki za wanawake na afya bora ya kuwa wakati umeshawadia kwa walimwengu kutimiza ahadi ya kuekeza mitaji ya maendeleo katika huduma za kustawisha afya na hali njema kwa wanawake kote duniani, ikijumuisha pia udhibiti wa vifo vya uzazi. Alionya Naibu KM kwamba bila ya kuyafanya haya mataifa yote, kote duniani, hayatofanikiwa abadan kujiepusha na athari za umasikini na hali duni.