Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

WFP imeshtumu mauaji ya madereva wake watatu katika Darfur

WFP imeshtumu mauaji ya madereva wake watatu katika Darfur

Shirika la Miradi ya Maendeleo Duniani (WFP) limetoa ilani yenye kulaani, kwa kauli moja, mauaji ya madereva watatu wa malori waliokodiwa kugawa vyakaula, ambao walipigwa risasi na watu wasiojulikana katika eneo la Darfur. WFP bado haijapokea taarifa yenye kuthibitisha ni makundi gani hasa yalioendeleza jinai hii. Kawaida WFP huajiri madereva wa muda na wasaidizi wao 2,000 katika Darfur, ambao hutumiwa kuhudumia chakula watu milioni tatu, kuwakilisha operesheni kubwa kabisa ya shughuli hizi duniani.