Mnyarwanda aliyeshtakiwa mauaji ya maangamizi amekamatwa Ufaransa
Mapema wiki hii Serikali ya Ufaransa imemkamata raia wa Rwanda, Dominique Ntawukuriryayo katika mji wa Carcassone, Ufaransa kusini ambaye alituhumiwa kushiriki kwenye mauaji ya halaiki katika jimbo la Butare, Rwanda kusini mnamo miaka ya 1990.