Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mkurugenzi wa UNDP asifu maendeleo ya uchumi Afrika kusini ya Sahara

Mkurugenzi wa UNDP asifu maendeleo ya uchumi Afrika kusini ya Sahara

Kemal Dervis, Mkurugenzi Msimamizi wa UNDP karibuni alifanya ziara ya siku 10 katika Msumbiji, Rwanda na Tanzania. Aliporejea Makao Makuu aliitisha mkutano na wanahabari wa kimataifa katika mwanzo wa wiki na alielezea kwamba ule mfumo wa kuambatanisha utekelezaji wa miradi ya mashirika ya UM chini ya mwongozo mmoja, kitaifa, unatekelezwa kwa taratiibu zenye kutia moyo sana katika zile nchi alizozitembelea.

Sikiliza maelezo kamili kwenye idhaa ya mtandao.