Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mwakilishi mpya wa KM kwa Sudan kawasili Khartoum

Mwakilishi mpya wa KM kwa Sudan kawasili Khartoum

Ashraf Jahangir Qazi, Mwakilishi Maalumu mpya wa KM kwa Sudan, ambaye pia ni mkuu wa Shirika la Ulinzi wa Amani la UM Sudan (UNMIS), amewasili Khartoum wiki hii na kutarajiwa kufanyisha msururu wa mikutano na maofisa wa ngazi ya juu wa Serikali, akiwemo vile vile Raisi wa Sudan Omar AlBashir na pia Makamu wa Kwanza wa Raisi na Raisi wa Serikali ya Sudan Kusini, Salva Kiir.